ADVERTISE WITH US HERE FOR YOUR OWN EXPANSION AND PROSPERITY

.
.

President of Tanzania hon Jakaya Kikwete

President was greeting the official during the 47th commemorations of the United republic of Tanzania that was held in Tanzania Islands of Zanzibar .Picture by rahma Hashim-Mgonjahmedias.

The beautful buildings of the central bank of the united republic of tanzania

These two twin buildings are of the ministry of finance in Tanzania.

Advertise with us today and expand your prosperity

Contact us today and Advertise your buisness or any other thing and earn more revenue.

Advertise with us today and expand your prosperity

Contact us today and Advertise your buisness or any other thing and earn more revenue.

President of Tanzania Hon.Jakaya Kikwete

The 47th commemorations of the United republic of Tanzania. Picture by Jacquelin Jackson - MgonjahMedias.

President of the united republic of Tanzania Hon.JK together with the military commanders

This was the 47th commemorations of the united republic of Tanzania and the President was inspecting the Guards prepared by the Tanzania Peoples Defence force(TPDF),It was held in Tanzania Islands.Picture by Mponela Mathei -MgonjahMedias.

Tuesday, December 6, 2011

Tangazo La nafasi za kazi kwa wenye Vigezo

POWER SYSTEM MANAGER
Qualification: Advanced Diploma in Electrical Engineering  or 
equivalent
Apply: Power Generation 
Services Ltd
Box 11609, Dar es Salaam
Details: Daily News 
November 04, 2011
Deadline: November  30, 2011


DIRECTOR OF COMPLIANCE
Qualification: Holder of Master’s degree in the field of Law from any recognized University
Apply: Director General Fair 
Competition Commission
Box 7883 , Dar es Salaam
Details: Daily News 
November 04, 2011
Deadline: November  30, 2011

DIRECTOR OF CORPORATE AFFAIRS
Qualification: Holder of Master’s degree in the field of Management, Finance,Business Administration or Law from any recognized University
Apply: Director General Fair 
Competition Commission
Box 7883 , Dar es Salaam
Details: Daily News 
November 04, 2011
Deadline: November  30, 2011

IT MANAGER
Qualification: Bachelor of Computer Science /Bachelor of Coputer Engineering or Equivalent
Apply: Head Office, IMMMA house
Box  72484 , Dar es Salaam
Details: Daily News 
November 02, 2011
Deadline: November  30, 2011

FINANCE AND ADMINISTRATION INTERN 
Qualification: Bachelor degree in accounting ,
Finance or Business Administration
Apply:http://www.engerhealth.org
Details: Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011
 
ASSISTANT ACCOUNTANT GRADE I DUTY STATION DAR ES SALAAM
Qualification: FForm VI with intermediate
qualification at the level of ADA, B.Com with module D or equivalent
Apply:Director General , T Tea board of Tanzania Box 2663 , Dar es Salaam Details:
Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011
 
SENIOR SUPPLIES OFFICER GRADE II DUTY STATION DAR ES SALAAM
Qualification: Holder of Degree in Materials Management and Supplies or Advanced Diploma in Materials Management and Supplies or Procurement and Supply/Logistics recognized by National Board of Materials Management
Apply:Director General , Tea board of Tanzania Box 2663 , Dar es Salaam
Details: Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011
 
ZONAL TEA INSPECTORS 2 POSTS DUTY STATIONS IRINGA AND TANGA
Qualification: Holder of Bsc.Degree in either Agriculture,Food Processing or Process Engineering from a recognized institution or its equivalent
Apply:Director General , Tea board of Tanzania Box 2663 , Dar es Salaam
Details: Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011

PROFESOR
Qualification: Possession of Form IV or VI Certificate with credit in Biology plus a training cource in dissection / n /embalming
Apply:The Provost Kilimanjaro Christian Medical College Box 2240 , Moshi
Details: Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011

LABORATORY ASSISTANTS
Qualification: Certificate in Health Laboratory Sciences or in Medical Laboratory Technology from a recognized institution
Apply:The Provost Kilimanjaro Christian Medical College Box 2240 , Moshi
Details: Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011

LABORATORY TECHNICIANS
Qualification: Diploma in Health Laboratory Sciences or Medical Laboratory Technology from a recognized institution Apply:The Provost Kilimanjaro Christian Medical College Box 2240 , Moshi
Details: Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011

PERSONAL SECRETAR ETARY ARY ETAR
Qualification: Diploma in Secretarial Studies conducted by the Tanzania Public service college
Apply:The Provost Kilimanjaro Christian Medical College Box 2240 , Moshi
Details: Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011

OFFICE MANAGEMENT ASSISTANT
Qualification: Advanced Dip[loma or degree in Secretarial Studies
Apply:The Provost Kilimanjaro Christian Medical College Box 2240 , Moshi
Details: Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011

SENIOR PROCUREMENT & SUPPLIES OFFICER
Qualification: Master degree in Materials Management,Procurement and Supply Management, CSP,CPSP,CIPS or equivalent Apply:The Provost Kilimanjaro Christian Medical College Box 2240 , Moshi
Details: Daily News Nov 16, 2011
Deadline: November 30, 2011  
ATIVE OFFICER 2 POSTS A ADMINISTRATIVE
Qualification: Holder of a first degree in Human Resources Management Business Administration or Public Administration Socialogy or equivalent
Apply:The Deputy Vice Chancellor,Planing Finance and Administra sity of Health sit tion,Muhimbili University and Allied Sciences Box 65001 , Dar es Salaam
Details: Daily News Nov 10, 2011
Deadline: November 26, 2011

 ADMINISTRATIVE OFFICER
 Qualification: Holder of a Bachelors degree in Health Administration , Business Administration or Public Administration or Health systems Management
 Apply:The Deputy Vice Chancellor,Planing Finance and Administration,Muhimbili University of Health and Allied Sciences Box 65001 , Dar es Salaam
 Details: Daily News Nov 10, 2011
 Deadline: November 26, 2011 


 OCCUPATIONAL HEALTH SUPERINTENDENT
 Qualification: Degree in in Science or Engineering
 Apply: recruitment@barrick.com Details: Daily News Nov 08, 2011
 Deadline: November 25, 2011


 DIRECTOR OF CORPORATE AFFAIRS
 Qualification: Master's degree in Business /Public Administration /Management ( MBA/MPA/MAM)
 Apply: Manpower Services (T) LTD, Management Training and Recruitment Consultant Box 9341 , Dar es Salaam
 Details: Mwananchi Nov 09, 2011
 Deadline: December 08, 2011

TUTORIAL ASSISTANTS PHTS 9-12 ( 2 POSITIONS )
Qualification: Holders of a Bachelors degree from a recognized higher learning institution
 Apply: Chairperson Appointments Committee,Centre for Foreign Relations Box 2824 , Dar es Salaam Details: Mwananchi Nov 09, 2011
 Deadline: December 02, 2011


 ASSISTANT LECTURERS PHTS 13-14 ( 5 POSITIONS )
 Qualification: Holders of a Masters degree from a recognized higher learning institution
 Apply: Chairperson Appointments Committee,Centre for Foreign Relations Box 2824 , Dar es Salaam
 Details: Mwananchi Nov 09, 2011
 Deadline: December 02, 2011
 


 SENIOR LECTURES PHTS 18-19 ( 3 POSITIONS )
 Qualification: Holders of a PhD from a recognized higher learning institution plus Masters and Bachelors degree
 Apply: Chairperson Appointments Committee,Centre for Foreign Relations Box 2824 , Dar es Salaam
 Details: Mwananchi Nov 09, 2011
 Deadline: December 02, 2011


 GRANTS COORDINATOR
 Qualification: Master's degree in project Management or equivalent
 Apply: HResource@wwfesarp.org
 Details: Mwananchi Nov 09, 2011
 Deadline: November 23, 2011
 
 POWER SYSTEM MANAGER
 Qualification: Advanced Diploma in Electrical Engineering or equivalent
 Apply: Power Generation Services Ltd Box 11609, Dar es Salaam
 Details: Daily News Nov 04, 2011
 Deadline: November 30, 2011


 DIRECTOR OF COMPLIANCE
 Qualification: Holder of Master's degree in the field of Law from any recognized University
 Apply: Director General Fair Competition Commission Box 7883 , Dar es Salaam
 Details: Daily News Nov 04, 2011
 Deadline: November 30, 2011


 DIRECTOR OF CORPORATE AFFAIRS
 Qualification: Holder of Master's degree in the field of Management, Finance,Business Administration or Law from any recognized University
 Apply: Director General Fair Competition Commission Box 7883 , Dar es Salaam
 Details: Daily News Nov 04, 2011
 Deadline: November 30, 2011


IT MANAGER
Qualification: Bachelor of Computer Science /Bachelor of Coputer Engineering or Equivalent
Apply: Head Office, IMMMA house Box 72484 , Dar es Salaam
Details: Daily News November 02, 2011
Deadline: November 30, 2011

Chanzo cha habari hii ni mwananchi
follow us onFacebook

Nchi za Marekani na Uchina Zachangamkia Kiswahili

UKISIKILIZA watu kutoka nje ya Tanzania wanavyozungumzia nafasi ya Kiswahili kwenye ulingo wa kimataifa, utakubaliana moja kwa moja na usemi kuwa  nabii hakubaliki kwao.

Wakati kukiwa na idadi kubwa ya  raia wa kigeni wanaokuja nchini  kujifunza lugha ya Kiswahili, bado Watanzania hawaithamini lugha yao kiasi kwamba mpaka sasa hawajaona umuhimu wa kuitumia lugha hiyo kufundishia katika madaraja yote ya elimu.
Baadhi ya wanafunzi kutoka mabara ya Asia na Amerika  wanaosoma Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,   wanaeleza sababu zilizowasukuma kuja kusoma Kiswahili na nafasi ya lugha hiyo kimataifa.Wanafunzi wa mwaka wa tatu kutoka Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Tianjin cha nchini  China, wanasema wamechagua kusoma Kiswahili kwa sababu wanajua kwa siku za usoni kitakuja kuwa moja ya lugha kubwa duniani.

Wanafunzi hao  wanasema  kwa kipindi cha miaka miwili walikuwa wakijifunza lugha hiyo kupitia walimu kutoka Zanzibar na China.Wang Panlolei  ambaye baada ya kufika nchini,  mwalimu wake alimpa jina la Aisha kutokana na kushindwa kutaja jina lake la asili, anasema ameamua kujifunza Kiswahili kwa sababu Tanzania ni moja ya nchi zinazoendelea kama ilivyo China.

“Nilipotakiwa kuchagua lugha nitakayosoma,  niliingia kwenye mtandao ndiyo nikaona Kiswahili, Nikaona  ni lugha inayozungumzwa na watu wa Afrika Mashariki na nilipenda utamaduni wa watu hawa. Kutokana na hali hiyo nikaamua kusoma Kiswahili,” anasema na kuongeza:
“Nilikuwa nafuatilia sana habari za Kiswahili kwenye mtandao na katika kutafuta habari,  niliona mpaka gazeti la Mwananchi na wakati mwingine nikawa nalitumia kupata habari za Kiswahili.”

Anaeleza kuwa  mbali na gazeti hili, pia hutumia Redio za BBC na Kiswahili China Radio International kujifunza lugha ya Kiswahili.Hata hivyo anasema kuwa Kiswahili alichojifunza kwa miaka miwili nchini China ni tofauti na kile wanachokitumia  Watanzania hasa katika mazungumzo.


“Kule sisi tunajifunza sana sarufi na pia hatupati nafasi kubwa ya kuzungumza Kiswahili…, ukisoma kwenye kitabu unaambiwa ukitaka kumsalimia mtu unamwambia ‘hujambo’, lakini ukija huku watu wanasalimiana ‘mambo, ’” anasema mwanafunzi huyo.Kuhusu nafasi ya Kiswahili kimataifa, anasema  hakuna ubishi kuwa Kiswahili ndiyo lugha ya Kiafrika.

“Kiswahili ni lugha ya kipekee,  ina nafasi sana ya kuwa lugha kubwa kama zilivyo nyingine duniani, lakini bado inatakiwa kipewe nafasi kubwa kama kufundishia shule za sekondari, vyuoni na pia kitangazwe zaidi,” anaeleza.
Naye Wu Zhen Huan ama Bakari kama anavyojulikana kwa walimu wake, anasema aliijua lugha ya Kiswahili kupitia mtandao baada ya  kuvutiwa na utamaduni wa watu wake.

“Lugha ni sehemu kubwa ya utamaduni wa mtu, kwa hiyo najua mpaka nikihitimu shahada yangu ya Kiswahili nitakuwa nimeijua sehemu kubwa ya utamaduni wa Watanzania,” anasema.

Anasema ili kuendeleza utamaduni wa Kitanzania, Serikali haina budi kuongeza juhudi za kuitangaza lugha ya Kiswahili na kuitumia kama lugha ya kufundishia katika elimu kama ilivyo China.

Kwa upande wake,  Ye Tianfa au Suleiman  anasema ni Watanzania wenyewe watakao weza kukiinua Kiswahili kwa kukipenda na kukithamini.Pia Yu Shaoshuai ama Hamisi, anasema aliamua kujifunza Kiswahili baada ya kushindwa kuelewana na wafanyabiashara wengi kutoka Afrika Mashariki wanaokwenda kununua bidhaa katika mji wa Yiwu mji ambao ndiko anakotoka.

“Nikimaliza shahada  yangu ya Kiswahili, nitafanya biashara vizuri kwa sababu nitakuwa sisumbuliwi tena na lugha hii,” anasema Shaoshuai.Naye  Zhu Chanjiao anayeitwa pia kwa jina la Lulu, anasema sababu kubwa ya kujifunza Kiswahili ni kutokana na kiu yake ya kueneza utamaduni wa Kichina katika nchi za Afrika Mashariki.

“Nikimaliza chuo najua nitakuwa na nafasi nzuri ya kueneza utamaduni wetu wa China Afrika Mashariki kwa sababu lugha itakuwa hainisumbui,” anabainisha.

Wanafunzi hao wanaosoma kwa  ufadhili wa pamoja wa Serikali za China na Tanzania, watatumia muda wa miezi nane kujifunza Kiswahili kabla ya kurejea kwao kumaliza masomo yao.

Mwanafunzi mwingine,  Chris Vavdo kutoka Marekani, anasema japo kwa sasa Kiswahili hakina nafasi  katika  kimataifa kikilinganishwa na lugha kama Kiingereza, au Kifaransa, anatoa rai kwa Watanzania kuanza kukipandisha chati kwa kuitumia kama lugha kuu katika elimu.
Kwa mujibu wa Taasisi ya Taaluma ya Kiswahili ya chuo hicho(Tataki), idadi kubwa ya wanafunzi kutoka nje ya nchi wanaosoma Kiswahili kwenye taasisi hiyo, wanatoka nchi za China na Marekani.

Tataki inasema ushirikiano wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na vyuo vingine vya nje, ni moja ya sababu inayoongeza idadi ya wanafunzi wanaosoma Kiswahili katika taasisi hiyo.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa anasema  sera ya elimu inayoendelea kuandaliwa, italeta mabadiliko mbalimbali katika elimu ikiwamo kukipa hadhi Kiswahili

Akifafanua anasema  katika mabadiliko hayo, lugha ya kufundishia katika madaraja ya sekondari na msingi itakuwa Kiswahili na Kiingereza tofauti na sasa ambapo kwa upande wa sekondari lugha inayotumika ni  Kiingereza pekee.
Kwa mujibu wa Dk Kawambwa,  shule za awali zitatumia Kiswahili huku vyuo vya ualimu  vikitumia  Kiswahili na Kiingereza. “Shule nyingine zitatumia Kiingereza na nyingine zitaruhusiwa kutumia Kiswahili kwa upande wa sekondari,” anasema
Na Mwananchi
Posted By MgonjahMedias Team Edited by AmanyMei-Xing ZachariƩliz
Follow us on Facebook

UIngereza Yailipa Tanzania Mabilion ya Shiling kwa kashfa ya Rada

Bank kuu ya Tanzania BOT yapokea pesa za mabilion ya rada ktoka Uingereza.Serekali yashauriwa kuwaburuza wahusika wa Kashfa hiyo mahakamani.
Na Mwananchi
BAADA ya vuta nikuvute ya muda mrefu kuhusu kurejeshwa fedha za ziada zilizotumika katika ununuzi wa rada, hatimaye Serikali ya Uingereza imeingiza Sh29.5 bilioni kwenye akaunti ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), tawi la Uingereza kama marejesho ya fedha hizo.Uamuzi huo wa Uingereza kurejesha fedha hizo, unakwenda sambamba na ombi lake la kutaka watuhumiwa wote wa hapa nchini waliohusika na ununuzi wa rada hiyo mtumba kutoka Kampuni ya BAE Systems, washitakiwe Tanzania au Uingereza baada ya kubainika dosari kwenye ununuzi huo ambao kama ungefanyika kihalali ungehitaji Pauni  10.5 milioni, kununua rada mpya.

Akizungumza na gazeti katika mahojiano maalumu jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Fedha, Mustapha Mkulo, alisema fedha hizo tayari zimekabidhiwa kwa tawi hilo la BoT nchini Uingereza ili ziweze kurejeshwa nchini.

Waziri Mkulo alisema kutokana na masharti waliyopewa, Serikali imekusudia kupeleka fedha hizo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ili ziweze kutatua matatizo mbalimbali yanayoikabili sekta ya elimu nchini.

‘’Tulikaa na kujadili namna ya matumizi ya fedha hizo kutokana na masharti tuliyopewa, jambo ambalo limesababisha tuamue kuziwasilisha Wizara ya Elimu ili kutatua changamoto zilizopo,’’ alisema Waziri Mkulo.

Aliongeza kwamba kutokana na hali hiyo, Wizara ya Elimu tayari imewasilisha mchanganuo wa matatizo yaliyopo na kiasi cha fedha zinazohitajika ili ziweze kupitishwa kwa matumizi.

Kwa mujibu wa Mkulo, kinachosubiriwa sasa ni kikao cha majadiliano kati ya wizara yake, Wizara ya Elimu, Wizara ya Mambo ya Nje Ushirikiano wa Kimataifa na Ubalozi wa Uingereza ili kuweza kupanga namna bora ya matumizi ya fedha hizo.

Alisema kutokana na hali hiyo, wanaamini matatizo mengi yanayoikabili Wizara ya Elimu yatapunguzwa kwa fedha hizo. Mengine yanayoweza kupatiwa ufumbuzi ni pamoja malalamiko ya madai ya walimu, uhaba wa vitendea kazi na mahitaji mengine ya wizara hiyo.

"Tulikaa na kujadili changamoto zinazoikabili sekta ya elimu, jambo ambalo limetufanya tuipitishe katika matumizi ya fedha hizi, kutokana na hali hiyo tunasubiri kibali cha Ubalozi wa Uingereza ili tuweze kuzichukua na kuzitumia kama ilivyokusudiwa,’’ alisisitiza Waziri Mkulo.


Siri zaidi

Wakati Uingereza ikitaka watuhumiwa hao wafikishwe mahakamani, kashfa nyingine imeikumba Serikali ya Tanzania ikituhumiwa kwamba ina mkakati maalumu kuzuia watuhumiwa wa ufisadi wa rada kufikishwa mahakamani.

Taarifa za mtandao wa Wikileaks ambao umekuwa ukifichua siri za kidiplomasia na ufisadi duniani, umeibua tuhuma hizo mpya kwa Serikali na kwamba hicho ndicho kikwazo cha watuhumiwa husika kutofikishwa mahakamani.

Taarifa ya mtandao huo iliyosambazwa hivi karibuni, imeeleza kuwa mpango huo ndiyo ulioathiri jitihada za aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa (DFID) Clare Shot aliyepinga BAE Systems kuizia Tanzania rada hiyo kuukuu kwa bei ghali wakati ni nchi masikini inayotegemea misaada ya wahisani.

Kwa mujibu wa mtandao huo, juhudi za Shot zilijumuisha kuinyima Tanzania misaada inayofikia Pauni 35 milioni kutokana na kununua rada hiyo kwa bei ya kuruka.

"Pamoja na shinikizo hilo, juhudi za Shot zilishindwa kabisa kuzuia ununuzi wa rada hiyo ambayo thamani yake ilikuwa Pauni 28 milioni kutoka kwa kampuni ya BAE Systems ya Uingereza," ulisema mtandao huo na kuendelea:

"Suala hilo si jipya. Gazeti la The Guardian la Uingereza liliwahi kutoa ripoti ya uchunguzi wake kuhusu uuzwaji wa rada hiyo ambao ulimsababishia pia Waziri Mkuu wa Uingereza wakati huo, kisha Tony Blair akiwa Waziri Mkuu wa nchi aliamuru kikosi chake cha Kuchunguza Makosa Makubwa (SFO), kuingilia kati na kuchunguza namna BAE ilivyohusika."

Ilichobaini Wikileaks ni kwamba, viongozi wa Serikali ya Tanzania walikuwa wakifanya juhudi za kuficha kasoro zote zilizokuwa katika mpango wa ununuzi wa rada hiyo.

Hata kwa upande wake, mtu mahususi aliyetakiwa kushughulikia kashfa hiyo kwa kufanya uchunguzi ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( Takukuru), Dk Edward Hoseah alinukuliwa akimweleza Ofisa wa Ubalozi wa Marekani nchini kwamba, aliwahi kutishiwa kuuawa mara kadhaa na kukumbushwa kwa ujumbe wa maneno kila siku.

BAE Systems ni kampuni kubwa ya uuzaji wa vifaa vya ulinzi ambayo iwapo ingefungiwa kufanya biashara yake, kungekuwa na athari kubwa kwa Uingereza.

Suala la uchunguzi wa aina yoyote ambao ungemweka matatani Rais wa zamani, Benjamin Mkapa na washirika wake wa karibu (kwa mujibu wa Wikileaks), lilikuwa ni gumu kuweza kufanyika.

Ulisema baada ya kumalizika kwa kipindi cha ukimya bila kushughulikiwa kwa kashfa hiyo, suala la kutafuta ufumbuzi lilionekana kuwa muhimu kwa nchi zote mbili, lakini kasoro kubwa ni pale kila aliyehusika katika kashfa hiyo ya BAE nchini Uingereza na Tanzania, kukwepa kuchunguzwa.

Hata hivyo, Blair alifanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba SFO wanafanya uchunguzi na kwamba, ikiwezekana BAE ifungiwe kufanya kazi katika nchi za Umoja wa Ulaya.

Kwa upande wake, Tanzania ilikuwa ikilaumiwa kwa kufanya juhudi za kutetea ununuzi huo na hata kumtisha Mkurugenzi wa Takukuru kumtaka aachane na suala hilo.

Dk Hosseah
Mtandao wa Wikileaks ulidai kuwa Dk Hoseah, ameshindwa kuwafikisha mahakamani vigogo waliohusika na kashfa ya rada kwa sababu anahofia usalama wake.
Mbali na hofu hiyo, mtandao huo ulieleza kuwa Dk Hoseah alipewa maelekezo maalumu na Rais Kikwete, kutoshughulikia kesi za rushwa zinazowahusu vigogo katika Serikali yake na hasa marais waliomtangulia.

The Guardian lilitoa taarifa hiyo likiunukuu mtandao wa habari wa WikiLeaks uliojizolea umaarufu duniani kwa kutoa habari za kiuchunguzi hasa baada ya mwasisi wake, Julian Paul Assange, kutiwa matatani.

Akijibu hoja hizo mwaka jana, Dk Hoseah alisema ni kawaida kwake kukutana na mabalozi wa nchi mbalimbali kila mwaka na kujadiliana nao mambo mengi kuhusu Tanzania, lakini hakumbuki kuzungumza naye mambo hayo.

Alisema mabalozi ni wadau wakubwa katika bajeti ya Tanzania na hivyo huwa wanakutana kila mwaka kujadili mambo mbalimbali kuhusu kusaidia bajeti ya Serikali.

“Mimi huwa nakutana na mabalozi wa nchi mbalimbali kwa sababu wao ni wadau katika mradi wa ‘Government  Budget Support’ (Mpango wa Kusaidia Bajeti ya Serikali), hivyo hilo sio tatizo,” alisema Dk Hoseah

“Msimamo wangu ni kwamba mapambao dhidi ya ufisadi ni endelevu hadi hapo tutakapofanikiwa kumaliza tatizo hili,” alisema Dk Hosea na kukiri:

“Vitisho vipo vingi tu, kutoka kwa watu wanaotuhumiwa, lakini si hata ninyi waandishi mnamwagiwa ‘tindikali’ katika mapambano yenu, hivyo hivyo hata mimi napata vitisho.”

Lakini alisisitiza kuwa pamoja na vitisho hivyo, hawezi kurudi nyuma katika mapambano ya rushwa na ufisadi.

“I’m a Tanzanian, I will die in Tanzania, it is my country’ (mimi ni Mtanzania, nitafia Tanzania, ni nchi yangu), siwezi kuhama nchi kwa vitisho vya watu wachache wanaotuhumiwa kwa ufisadi na rushwa,” alisisitiza Dk Hoseah.

Kuhusu Rais Kikwete kukwamisha mapambano ya ufisadi kama alivyonukuliwa na gazeti hilo la The Guardian, Dk Hoseah alipiga chenga kulijibu akisema:

“Ili umpeleke mtu mahakamani si lazima umtuhumu na kumfanyia uchunguzi? Lakini pia lazima tujenge utamaduni wa kuwaheshimu viongozi wetu.”

Siku hiyo, Takukuru ilituma taarifa iliyoeleza kuwa Dk Hoseah alishangazwa na Ofisa wa Ubalozi wa Marekani kumnukuu vibaya huku akisema hajui ana lengo gani.

Katika taarifa hiyo, Dk Hoseah alikiri kukutana na ofisa huyo wa Ubalozi wa Marekani ofisini kwake Julai mwaka 2007, lakini akasema ripoti ya mazungumzo yao aliyoipeleka nchini kwake imechakachuliwa.

“Kwa mfano haikutokea katika mazungumzo yetu kusema kwamba Rais Jakaya Kikwete hakutaka kuruhusu sheria kuchukua mkondo wake, kuwashitaki vigogo wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi kama ilivyodaiwa na Ubalozi wa Marekani,” ilisema taarifa hiyo iliyotolewa na Idara ya Uhusiano ya Takukuru.

Bunge la Uingereza
Taarifa ya mtandao huo ilikuja siku moja tangu Bunge la Uingereza liitake Serikali ya Tanzania kuwafikisha mahakamani watu wote walioshiriki mchakato wa ununuzi wa rada na kuingiza nchi katika hasara ya mabilioni ya fedha.

Kupitia Kamati yake ya Maendeleo ya Kimataifa, Bunge hilo lilisema lingependa kuona watu wote walioshiriki kwenye mchakato wa ununuzi wa rada hiyo, wakifikishwa mahakamani kujibu tuhuma za ufisadi.  
Taarifa ya kamati hiyo iliyonukuliwa na Shirika la Habari la Uingereza (BBC), ilieleza kuwa wajumbe wake ambao ni wabunge kutoka vyama mbalimbali, watatoa ushirikiano wa dhati kwa Tanzania iwapo itaamua kuwashtaki watuhumiwa hao nchini Tanzania au Uingereza.

Wito huo wa wabunge wa Uingereza umekuja wakati tayari Kampuni ya BAE System, iliyoiuzia Tanzania rada hiyo, ikikubali kuwa kulikuwa na kasoro katika mchakato wa ununuzi wa rada hiyo, hivyo kuirudishia Tanzania Dola za Marekani 46 milioni kama fidia.  
Shukrani kwa  Mwananchi
Posted By Mgonjahmedias Team
Edited by Jacquelin Jackson
Follow us on Facebook

Subscribe